2 Samweli 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.
Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’