2 Samweli 23:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20028 Haya ni majina ya mashujaa Daudi aliokuwa nao: Yosebu-Basebeti, wa muji wa Takemoni ndiye aliyekuwa kiongozi wa wale watatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake, akaua watu mia nane mara moja katika vita. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Walikuwa chini ya usimamizi wa wakubwa hawa: Mwezi wa kwanza: Yasobeamu mwana wa Zabudieli, wa uzao wa Peresi. Alikuwa mukubwa wa majemadari wote wa jeshi katika mwezi wa kwanza. Mwezi wa pili: Dodayi wa Ahoa. Alisaidiwa na jemadari Mikiloti. Mwezi wa tatu: Benaya, mwana wa Yehoyada aliyekuwa Kuhani Mukubwa. Huyu ndiye Benaya aliyekuwa mutu shujaa katika kundi la watu makumi tatu na kiongozi wa kundi lile. Naye Amizabadi mwana wake, alikuwa jemadari. Mwezi wa ine: Asaheli, ndugu ya Yoabu, na nyuma yake alifuatwa na Zebadia mwana wake. Mwezi wa tano: Samuhuti wa uzao wa Isira. Mwezi wa sita: Ira mwana wa Ikesi wa muji wa Tekoa. Mwezi wa saba: Helesi wa muji wa Peloni, wa uzao wa Efuraimu. Mwezi wa nane: Sibekayi wa muji wa Husati, wa uzao wa Zera. Mwezi wa kenda: Abiezeri wa muji wa Anatoti wa uzao wa Benjamina. Mwezi wa kumi: Maharai wa muji wa Netofati wa uzao wa Zera. Mwezi wa kumi na moja: Benaya wa muji wa Piratoni. Mwezi wa kumi na mbili: Heldai wa muji wa Netofati, wa uzao wa Otinieli.