30 Benaya wa muji Piratoni; Hidayi wa vijito vya Gasi;
Watu hao wakakwenda katika inchi ile ya milima, wakafika kwenye bonde la Eskoli na kulipeleleza.
Nao wakamuzika kwenye eneo ambalo alikuwa amegawanyiwa kuwa sehemu yake, kule Timunati-Sera, katika milima ya Efuraimu, upande wa kaskazini wa mulima wa Gasi.
Nyuma ya Eloni, Abudoni mwana wa Hileli wa muji wa Piratoni akakuwa mwamuzi wa Israeli.
Kisha Abudoni akakufa, akazikwa katika muji wa Piratoni katika inchi ya kabila la Efuraimu kwenye eneo la milima ya Waamaleki.
Wakamuzika katika sehemu aliyogawanyiwa ikuwe yake kule Timunati-Heresi, katika inchi ya milima ya Efuraimu upande wa kaskazini wa mulima Gasi.