Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 23:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Alikuwa na heshima zaidi kati ya wale mashujaa makumi tatu. Kwa hiyo akakuwa jemadari wao, lakini hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 23:19
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu waliteremuka wakati wa mavuno, wakamufikia Daudi kwenye pango kule Adulamu. Wakati ule kundi la waaskari wa Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.


Wale mashujaa wake watatu walitoka, wakapenya katikati ya kambi ya kundi la waaskari wa Wafilistini, wakaenda na kuchota maji katika kisima cha Betelehemu, karibu na mulango wa muji, wakamuletea Daudi. Lakini Daudi alikataa kuyakunywa, na pahali pa kuyakunywa, akayamwanga chini kama vile sadaka kwa Yawe,


Abisayi mwana wa Zeruya na ndugu ya Yoabu alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia sifa pamoja na wale mashujaa watatu.


Naye Benaya mwana wa Yehoyada wa muji Kabuseli, alikuwa askari shujaa ambaye alifanya mambo mengi ya ajabu. Aliwaua mashujaa wawili kutoka Moabu, na siku moja wakati wa teluji, alishuka katika shimo na kuua simba.


Halafu aliyefuata kati ya wale mashujaa watatu alikuwa Eleazari mwana wa Dodayi, wa ukoo wa Muahoa. Siku moja, Eleazari alikuwa pamoja na Daudi walipowatukana Wafilistini waliokuwa wamekusanyika kwa kupigana vita. Waisraeli waliwakimbia Wafilistini.


Basi, akakuwa mwenye heshima kati ya wale mashujaa makumi tatu, ingawa hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu. Na Daudi akamupa cheo cha mukubwa wa walinzi wake wa kipekee.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika udongo muzuri ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulielewa. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda mia moja, wengine makumi sita na wengine makumi tatu.”


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri na kutoa matunda: zimoja zikazaa punje mia moja, zingine makumi sita na zingine makumi tatu.


Uzuri wa jua ni mbalimbali na uzuri wa mwezi, nao uzuri wa nyota ni mbalimbali, kwa maana hata nyota zinapishana uzuri vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ