Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.
Hawa ndio watu waliovuka muto Yordani katika mwezi wa kwanza, muto ulipokuwa umefurika pande zote na kuwatawanya watu kwa upande wa mashariki na magaribi ya muto.
Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.
Waisraeli wote walisikia kwamba Saulo alikuwa ameishinda kambi ya waaskari walinzi wa Wafilistini, na kwamba Wafilistini wanawachukia sana Waisraeli. Waliitwa kwenda kuungana na Saulo kule Gilgali.
Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”
Daudi akaondoka kule, akakimbilia kwenye pango karibu na muji wa Adulamu. Kaka zake na wandugu zake wengine waliposikia kwamba alikuwa pale, wote walikwenda kuungana naye.