Lakini Eleazari alisimama imara na kupigana na Wafilistini mpaka mukono wake uliposhindwa kupindika, ukabaki umebania upanga wake. Siku hiyo, Yawe alijipatia ushindi mukubwa. Nyuma ya ushindi ule, Waisraeli walirudi pahali Eleazari alipokuwa na kuteka vitu kutoka kwa Wafilistini waliouawa.
Siku moja Eleazari alikuwa pamoja na Daudi kule Pasi-Damimu, wakati Wafilistini walipokusanyika kupigana vita. Kule kulikuwa shamba lenye shayiri tele, lakini Waisraeli wakawakimbia Wafilistini.