Mulima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa sababu Yawe alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto ule ulipanda juu kama moshi wa furu kubwa na mulima wote ukatetemeka kwa nguvu.
Muangalie, Yawe mwenyewe anakuja tokea mbali! Amewaka hasira na moshi unafuka; midomo yake inaonyesha kasirani yake, maneno anayosema ni kama moto unaoteketeza.
Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa sababu wao wamesema jambo hilo, sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto. Nao watu hawa watakuwa kuni, na moto huo utawateketeza.