Toka magaribi mpaka mashariki, kila mutu atamwogopa Yawe na kutambua utukufu wake. Maana atakuja kama muto wenye kuporomoka mbio, muto unaosukumwa kwa upepo wa Yawe.
Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.
Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.