Muulize vilevile Amasa kama yeye si damu yangu. Tena Mungu aniue ikiwa simufanyi yeye kuwa jemadari wa kundi langu la waaskari tangu leo pahali pa Yoabu.’ ”
Kisha, mufalme akatoka, akaenda, akaikaa kwenye nafasi yake karibu na mulango. Watu wote walipoambiwa kwamba mufalme yuko kwenye mulango, wote walimwendea. Wakati ule, watu wote wa Israeli walikuwa wamekimbia, kila mumoja kwake.
Kisha, huyo mwanamuke akaenda kwa watu wote katika muji kwa hekima yake. Wakamukata Seba mwana wa Bikiri kichwa, wakakitupa inje kwa Yoabu. Kwa hiyo, Yoabu akapiga baragumu na kuwatawanya watu wake kutoka muji ule wa Abeli. Kila mutu akaenda kwake. Yoabu akarudi kwa mufalme Daudi, kule Yerusalema.
Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.
Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.
Yawe anasema; Nilikuwa tayari kujionyesha kwao wasiouliza habari zangu. Nilikuwa tayari kuwapokea wale wasionitafuta. Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu: Niko hapa! Niko hapa!
Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.
Ni vile anavyosema katika maandiko haya ya nabii Hosea: “Wale waliokuwa si watu wangu nitawaita sasa ‘Watu wangu.’ Taifa lile nililokosa kulipenda nitaliita sasa ‘Mupendwa wangu.’
Yawe, Mungu wenu, atawafanya kuwa wa kwanza kwa nguvu na sio wa mwisho. Mutaendelea mbele na sio kurudi nyuma kama mukishika amri zake ambazo ninawapa leo na kuwa waangalifu kwa kuzitimiza,
Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”