Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ninamwita Yawe anayestahili sifa anisaidie, nami ninaokolewa kutoka kwa waadui zangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 22:4
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati walipoanza kuimba na kusifu, Yawe akawavuruga akili waaskari Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri waliokuja kupigana na Yuda. Na waaskari wale wakashindwa.


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Ni nani anayeweza kutaja matendo ya Yawe? Ni nani anayeweza kumusifu kama anavyostahili?


Nitamutolea sadaka ya divai kwa kumushukuru maana ameniokoa. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Nitakutolea sadaka za shukrani. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Yeye amenitegea sikio, hivyo nitamwomba muda wote wa maisha yangu.


Kisha nikamulilia Yawe: “Ee Yawe, tafazali uniokoe!”


Yawe ni kikingio changu, kimbilio langu, mukombozi wangu, Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu.


Mumugeukie Mungu mupate kufurahi; nanyi hamutafezeheka hata kidogo.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Acha kifo kiwashitukie waadui zangu, washuke chini katika kuzimu wangali wazima; maana uovu umejaa katika mioyo yao.


Wewe unajua kutangatanga kwangu; unaweka machozi yangu ndani ya chupa. Yote yanakuwa katika kitabu chako.


Muimbe kwa ajili ya utukufu wa jina lake, mumusifu kwa utukufu!


Maana Yawe ni mukubwa, anasifiwa sana; anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


Ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila mutu anayemusihi Bwana, ataokolewa.”


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ