Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!
Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.
Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.
Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.
Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.
Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!