Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 22:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Matendo ya Mungu ni makamilifu. Ahadi ya Yawe ni ya kuaminika. Yeye ni ngao kwa wote wanaomukimbilia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 22:31
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!


Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.


Kwa hiyo munisikilize, enyi wenye ujuzi. Mungu hawezi kufanya uovu hata kidogo; Mungu Mwenye Uwezo hawezi kufanya kosa.


Ahadi yako ni hakika kabisa, nami mutumishi wako ninaipenda.


Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”


Yawe ni mwenye haki katika njia zake zote; ni mwema katika matendo yake yote.


Kwa musaada wako, ninashinda kundi la waaskari; kwa musaada wa Mungu wangu, ninaruka kuta.


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Utwae ngao yako na kikingio chako, uinuke ukuje kunisaidia!


Usikie maombi yangu, ee Yawe, Mungu wa majeshi! Unitegee sikio, ee Mungu wa Yakobo.


Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.


Maneno yote ya Mungu ni ya kuaminiwa. Yeye ni ngao yao wote wanaomukimbilia.


Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ