Kisha mufalme na watu wake walikwenda Yerusalema kuwashambulia Wayebusi waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo. Lakini wao wakamwambia: “Hautaingia ndani ya muji huu, maana vipofu na vilema watakufukuza.” Walimwambia hivyo maana walifikiri kwamba Daudi asingeweza kuingia katika muji ule.