Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 22:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 22:3
52 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Matendo ya Mungu ni makamilifu. Ahadi ya Yawe ni ya kuaminika. Yeye ni ngao kwa wote wanaomukimbilia.


Yawe anaishi! Asifiwe yeye kikingio changu! Atukuzwe Mungu, kikingio na mwokozi wangu.


Ameniokoa kutoka waadui zangu. Ee Yawe, ulinitukuza juu ya wapinzani wangu na kuniponyesha kutoka watesaji wakali.


Mungu anamujalia mufalme wake ushindi mukubwa; anamutendea mema muchaguliwa wake, ndiye Daudi na wazao wake milele.


Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Unaweza kuvuruga mipango ya masikini, lakini Yawe ndiye kimbilio lake.


Makaa ya moto yawaangukie; watumbukizwe katika mashimo, wasiinuke tena.


Ndimi zao ni hatari kama za nyoka; ndani ya midomo yao kuna maneno ya sumu kama ya piri.


Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.


rafiki yangu wa kweli, kimbilio langu, upango wangu, mukombozi wangu, ngao yangu, yule anayenilinda, yule anayeshinda mataifa na kuyaweka chini yangu.


Siku ya taabu atanificha ndani ya nyumba yake; atanificha katika hema lake, atanilinda salama juu ya mulima.


Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.


Wengi wanasema juu yangu: “Hautapata musaada wowote kwa Mungu.”


Wewe unanificha kwa kunilinda wakati wa taabu. Ninazungukwa na ukombozi wako.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Lakini wanaokimbilia kwako wafurahi wote, waimbe kwa shangwe siku zote. Uwalinde wanaolipenda jina lako, kusudi wapate kushangilia kwa sababu yako.


ningekimbilia pahali penye usalama, mbali na upepo mukali na zoruba.”


Wanapitapita huko na huko wakitafuta chakula, nao wasiposhiba wananguruma.


Ninakulilia kutoka miisho ya dunia, nikikuwa nimevunjika moyo. Uniongoze juu kwenye mulima ambako siwezi kujifikisha.


Kwa wengi nimekuwa mushangao, lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.


Atawatoa katika mateso na ukali, maana maisha yao ni ya bei kubwa kwake.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Usikie maombi yangu, ee Yawe, Mungu wa majeshi! Unitegee sikio, ee Mungu wa Yakobo.


Ee Mungu, watu wenye kiburi wamenishambulia; kundi la watu wakali lilitaka kuniua, wala halikujali wewe hata kidogo.


Yawe ni kikingio cha watu wanaoonewa; yeye ni kikingio katika nyakati za taabu.


Anauhukumu ulimwengu kwa haki; anayaamua mataifa kama vile inavyofaa.


Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Maneno yote ya Mungu ni ya kuaminiwa. Yeye ni ngao yao wote wanaomukimbilia.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitazikomesha kabisa kutoka pahali hapa sauti za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa. Nitayafanya hayo yote katika nyakati zenu, na mutayaona waziwazi.


roho yangu inamufurahia Mungu, Mwokozi wangu;


Ametuletea Mwokozi mwenye uwezo, toka ukoo wa mutumishi wake Daudi.


Aliahidi kutuokoa toka mikono ya waadui zetu, ndio wale wanaotuchukia.


Ndipo Yawe atakapouliza watu wake: Iko wapi ile miungu yenu, mulinzi muliyekimbilia usalama?


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


Lakini wakati Mungu Mwokozi wetu alipoonyesha wema wake na upendo wake kwa watu,


Kwa maana Mungu amemimia Roho Mutakatifu kwa uwingi juu yetu kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu.


Tena anasema: “Nitamutumainia Mungu.” Na tena anasema: “Mimi ni hapa pamoja na watoto Mungu alionipatia.”


Halafu Hana aliomba na kusema: Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu. Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu. Ninawachekelea waadui zangu; maana ninaufurahia wokovu wako.


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ