Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.
Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.
Yawe anamulinda kila mutu kwa haki yake na uaminifu wake. Leo Yawe alikutia katika mikono yangu, lakini mimi sikunyoosha mukono wangu juu ya yule ambaye ni muchaguliwa wa Yawe.