Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.
Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.
Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.
Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.
Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
Sasa, Mungu amewapatanisha ninyi naye, kwa njia ya kufa kwa Mwana wake kimwili, kusudi awawezeshe kuonekana mbele yake mukiwa watakatifu, bila kilema wala kosa lolote.
Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.