Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 22:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Alinileta, akaniweka kwenye nafasi ya usalama; aliniponyesha kwa sababu alipendezwa nami.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 22:20
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Isaka akakwenda pahali pengine na kuchimba kisima kingine. Lakini hicho hawakukigombania. Hivyo Isaka akakiita “Nafasi Pana”, akisema: “Sasa Yawe ametuachia nafasi, nasi tutastawi katika inchi hii.”


Lakini ikiwa Yawe hapendezwi nami basi, mimi niko tayari; na anitendee sawa vile anavyotaka.”


Umepanua njia yangu wala miguu yangu haikuteleza.


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Katika taabu yangu nilimwomba Yawe, naye akanisikia na kuniweka huru.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


Wote wanaoniona wananichekelea; wananizomea na kutikisa vichwa vyao.


Nitashangilia na kufurahia wema wako, maana wewe unaona taabu yangu, unajua huzuni yangu.


Wewe haukunitoa katika mikono ya waadui zangu; lakini umenisimamisha kwenye pahali pa usalama.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ