Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.
Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.
Waadui za Yawe watavunjwa vipandevipande; atanguruma juu yao kama radi mbinguni. Yawe ataihukumu dunia yote, atamupa nguvu mufalme wake, na atautukuza uwezo wa muchaguliwa wake.
Samweli alipokuwa anatolea ile sadaka ya kuteketezwa, Wafilistini walikaribia kuwashambulia Waisraeli. Lakini Yawe akatoa sauti kubwa ya ngurumo juu ya Wafilistini, na kuwavuruga Wafilistini, nao wakashindwa mbele ya Waisraeli.