Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:7
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme akamwambia Siba: “Basi, yale yaliyokuwa mali ya Mefiboseti sasa ni mali yako.” Siba akamwambia: “Ninashukuru, bwana wangu mufalme, nami ninaomba nipate kukubaliwa mbele yako siku zote.”


Mefiboseti mujukuu wa Saulo alikwenda vilevile kumupokea mufalme Daudi. Tangu siku ile mufalme alipoondoka Yerusalema mpaka wakati aliporudi salama, Mefiboseti alikuwa hajapata kunawa miguu yake, kukata ndevu zake wala hakujali kufua nguo zake.


Yonatani mwana wa Saulo alikuwa na mutoto aliyekuwa kilema wa miguu. Mutoto huyo aliitwa Mefiboseti. Mefiboseti alikuwa na umri wa miaka mitano wakati habari za kifo cha Saulo na Yonatani ziliposikilika kutoka Yezereheli. Kwa wakati ule, mulezi wake aliposikia kwamba Saulo na Yonatani waliuawa kule Yezereheli, akamukamata Mefiboseti na kukimbia naye. Lakini alipokuwa anakimbia kwa haraka, mutoto huyo alianguka na kuwa kilema.


Siku moja, Daudi aliuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebakia katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea mema kwa ajili ya Yonatani.”


Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.


Basi, Mefiboseti mwana wa Yonatani na mujukuu wa Saulo akaenda kwa mufalme Daudi, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme Daudi. Daudi akamwita: “Mefiboseti!” Naye akamujibu: “Ndiyo! Mimi mutumishi wako niko hapa.”


Daudi akamwambia: “Usiogope. Mimi nitakutendea mema kwa ajili ya baba yako Yonatani. Nitakurudishia yale mashamba yote yaliyokuwa ya babu yako Saulo. Nawe, utakula kwenye meza yangu siku zote.”


Mimi ninasema hivi: tii amri ya mufalme. Kwa sababu ya kiapo chako kitakatifu, usikate tamaa.


Kwa sababu Yonatani alimupenda Daudi kama roho yake, alifanya agano naye.


Yonatani akamwambia Daudi: “Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe mushuhuda kati yetu. Kesho au kesho kutwa, wakati kama huu nitamwuliza baba yangu. Ikiwa musimamo wake juu yako ni muzuri nitakuelezea.


tena usiache kuitendea jamaa yangu kwa uaminifu milele. Na Yawe atakapowateketeza waadui zako kutoka katika dunia,


Kwa mara ingine tena, Yonatani alimwambia Daudi aape kulingana na upendo wake kwake yeye Yonatani, maana alimupenda Daudi kama vile anavyojipenda yeye mwenyewe.


Halafu Yonatani akamwambia Daudi: “Uende na amani. Tumekwisha wote kuapa kwa jina la Yawe kwamba Yawe akuwe mushuhuda kati yetu milele, na kati ya wazao wangu na wazao wako milele.”


Hivyo unitendee mema maana umefanya agano nami, mimi mutumishi wako, mbele ya Yawe. Lakini, kama nimefanya kosa basi, uniue wewe mwenyewe. Kwa nini unipeleke kwa baba yako kusudi aniue?”


Hao wote wawili, wakafanya agano mbele ya Yawe. Daudi akabaki katika muji wa Horeshi na Yonatani akaenda zake kwenye nyumba.


Lakini uniapie kwa jina la Yawe kwamba hautawateketeza wazao wangu, wala kufuta kabisa jina langu katika jamaa ya baba yangu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ