Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Lakini Abisayi mwana wa Zeruya alikwenda kumusaidia Daudi. Abisayi alimushambulia yule Mufilistini na kumwua. Kwa hiyo, watu wakamwapia Daudi wakisema: “Hautakwenda tena nasi katika vita, kusudi usiizime taa ya ufalme katika Israeli.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:17
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa wandugu zangu wote wamenigeuka mimi mujakazi wako. Wanataka nimutoe katika mikono yao yule mutoto aliyemwua mwenzake kusudi wamwue kwa kuyaangamiza maisha ya ndugu yake. Hivyo, watamwua huyu ambaye sasa ndiye murizi. Wakifanya hivyo, watazimisha kabisa tumaini langu lililobakia, na mume wangu hataachiwa jina wala muzao katika dunia.”


Daudi akatuma waaskari wake kwa vita katika vikundi vitatu: sehemu moja ya tatu ikiwa chini ya uongozi wa Yoabu, sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Abisayi mwana wa Zeruya, ndugu ya Yoabu; na sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Itayi wa muji wa Gati. Kisha mufalme Daudi akawaambia wote: “Mimi mwenyewe vilevile nitakwenda pamoja nanyi.”


Lakini watu wakamwambia: “Hautakwenda. Maana, ikiwa tutakimbia, hawatajali kitu juu yetu. Ikiwa nusu yetu watakufa, hawatahangaika nasi vilevile. Lakini wewe ni wa lazima kuliko watu elfu kumi kati yetu. Kwa hiyo inafaa wewe ubaki katika muji na kutupelekea musaada ukiwa katika muji.”


Walinishambulia nilipokuwa katika taabu, lakini Yawe alinikinga.


Ee Yawe, wewe ni taa yangu. Yawe anafanya giza langu likuwe mwangaza.


Huyo mwana wa Solomono nitamwachia kabila moja, kusudi wakati wote mutu mumoja wa uzao wa mutumishi wangu Daudi akuwe anatawala Yerusalema, akuwe taa inayoangaza siku zote mbele yangu katika muji ambao nimeuchagua ukuwe pahali pa kuniabudia.


Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, Yawe alimupatia Abiyamu mwana atakayetawala nyuma yake, kuwa taa ya kuangaza Yerusalema na kuuweka imara Yerusalema.


Humo nitamuchipukiza mufalme shujaa wa ukoo wa Daudi. Kama vile taa inayowaka, nitamwimarisha mufalme niliyemuchagua.


wewe unayewapa wafalme ushindi, unayemwokoa mutumishi wako Daudi!


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.


Kisha, Yohana mwana wa Karea akazungumuza na Gedalia kwa siri kule Misipa, akamwambia: Uniruhusu niende nimwue Isimaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu yeyote atakayejua. Kwa nini kumwachilia yeye akuue na Wayuda wote waliokusanyika hapa watawanyike na Wayuda waliobaki waangamie?


Yoane alikuwa kama taa inayowaka na kuangaza, na ninyi mulipendezwa kufurahishwa na mwangaza wake kwa muda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ