Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Isibi-Benobi, mutu mumoja wa wazao wa majitu ambaye mukuki wake wa shaba ulikuwa na uzito wa karibu kilo tatu na nusu na aliyekuwa amejifungia upanga mupya, alisema atamwua Daudi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:16
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu,


Katika siku zile na hata kisha, kulikuwa majitu katika dunia ambao walikuwa wazao wa wana wa Mungu na wabinti za wanadamu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa wa zamani, na waliitwa Wanefili.


Nyuma ya hayo, kulitokea tena mapigano na Wafilistini kule Gobu. Kule, Sibekayi wa muji wa Husa alimwua Safu aliyekuwa mutu mumoja wa wazao wa Rafa.


Kisha kulitokea tena vita kule Gati ambako kulikuwa na mutu mumoja alikuwa murefu sana, na mwenye vidole sita katika kila mukono, na vidole sita katika kila muguu, jumla ya vidole vyake ilikuwa makumi mbili na ine. Yeye vilevile alikuwa wa uzao wa majitu.


Hao wane walikuwa wazao wa majitu kule Gati, nao waliuawa na Daudi pamoja na watumishi wake.


Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.


Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).


Lakini wenyeji wake ni wenye nguvu sana, na miji yao ni imara na mikubwa sana. Zaidi ya hayo, huko tuliona wazao wa Anaki.


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


(Hapo zamani hiyo inchi ya Ari ilikuwa imekaliwa na watu wengi, wenye nguvu na ambao walikuwa warefu kama vile Waanaki.


Kama vile Waanaki, watu hawa walijulikana vilevile kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.


Walikuwa watu wengi, wenye nguvu na warefu kama vile Waanaki. Lakini Yawe akawaangamiza mbele ya Waamori ambao walitwaa inchi yao wakaishi humo pahali pao.


(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)


Watu wenyewe ni warefu na wenye nguvu; ni Waanaki ambao kama vile munavyojua na kama vile mulivyosikia watu wanasema juu yao: ‘Nani anayeweza kuwashambulia?’


Hakuna mutu wa kabila la Anaki ambaye alibakia katika inchi ya Israeli; walibaki wachache tu katika miji ya Gaza, Gati na Asidodi.


Kalebu alizifukuza kutoka muji huo ukoo tatu za Anaki, ni kusema ukoo wa Sesayi, ukoo wa Ahimani na ukoo wa Talmayi.


Mupini wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa mufumaji wa nguo, na chuma cha mukuki huo, kilikuwa na uzito wa kilo saba. Ngao yake ilibebwa na mutu mwingine aliyemutangulia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ