Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Basi, watu wa Daudi wakaizika mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani katika inchi ya Benjamina, kule Zela katika kaburi la Kisi baba ya Saulo. Walifanya kila kitu ambacho mufalme aliamuru. Nyuma ya hayo, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akairudisha mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kule; na kisha wakakusanya mifupa ya vijana saba waliotundikwa.


Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Basi, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi, na ule ugonjwa mukali uliowapata Waisraeli ikakoma.


Abeneri alizikwa kule Hebroni na mufalme aliomboleza kwa sauti akiwa pembeni ya kaburi. Watu wengine wote walifanya vile vile.


Daudi akawaamuru vijana wake, nao wakawaua. Wakawakata mikono na miguu. Halafu wakawatundika juu ya muti pembeni ya kisima kule Hebroni. Lakini walikichukua kichwa cha Isiboseti na kukizika katika kaburi la Abeneri kule Hebroni.


Basi, wakamukamata Yona, wakamutupa ndani ya bahari na palepale bahari ikatulia.


Kisha yule malaika aliyeongea nami akaniambia kwa sauti: Wale farasi waliokwenda katika inchi ya kaskazini wameituliza kasirani ya Yawe.


Ninaagana naye kwamba yeye na wazao wake watakuwa makuhani milele kwa sababu aliona wivu kwa ajili yangu mimi Mungu wake, akawafanyia Waisraeli upatanisho.


na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.


Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.


Leo tutakapoagana, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Rakeli kule Zeleza katika inchi ya Benjamina. Hao watakuambia kwamba wale punda uliokuwa unawatafuta wamekwisha kupatikana. Baba yako ameacha kufikiri juu ya punda, lakini ana wasiwasi juu yako, akijiuliza kila mara: ‘Nitafanya nini juu ya mwana wangu?’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ