Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kisha, Risipa binti ya Aya alitwaa nguo ya gunia, akajitandikia juu ya jiwe kubwa. Alikaa pale tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati wa mvua ulipofika na kuinyeshea maiti. Wakati huo wote, aliwafukuza ndege na wanyama wa pori, usiku na muchana, kusudi wasifikie maiti hizo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:10
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo, atainua kichwa chako kusudi akutundike juu ya muti, nao ndege watakula mwili wako.”


Daudi alisikia yale Risipa binti ya Aya, habara ya Saulo aliyofanya.


Saulo alikuwa na habara mumoja aliyeitwa Risipa, binti ya Aya. Basi, wakati mumoja, Isiboseti akamwuliza Abeneri: “Kwa nini umelala na habara ya baba yangu?”


Lakini, Ahabu aliposikia maneno hayo, akapasua nguo zake, akavaa gunia peke yake, akafunga, akakuwa analala na gunia, na kwenda huko na huko kwa huzuni.


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Angalia jinsi nyama wanavyolia kwa huzuni! Makundi ya ngombe yanahangaika, kwa sababu yamekosa malisho; hata makundi ya kondoo yanateswa.


Mufurahi, enyi watu wa Sayuni, mushangilie kwa sababu ya Yawe, Mungu wenu, maana amewapa mvua zinazowafalia, amewapa mvua ya kutosha: mvua za kwanza na mvua za katikati kama pale mbele.


Muombe Yawe awape mvua za masika. Yawe ndiye anayeleta mawingu ya mvua; ndiye anayewapa watu mvua za manyunyu, na kustawisha mimea katika shamba kwa ajili ya wote.


yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.


na kubadilisha nguo zake za kitumwa. Atakaa muda wa mwezi muzima kwa kumwomboleza baba yake na mama yake. Kisha mwanaume huyo anaweza kumwoa.


“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Mufilistini akamwambia Daudi: “Kuja kwangu! Mwili wako nitawapa ndege na nyama wa pori!”


Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ