Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 21:1
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda.


Kisha kukatokea njaa katika inchi ile, nyuma ya ile ya kwanza iliyokuwa kwa wakati wa Abrahamu. Isaka akakwenda Gerari kwa Abimeleki mufalme wa Wafilistini.


Zaidi ya hayo, watu toka kila pahali katika dunia walikuja Misri kwa Yosefu kununua ngano, maana njaa ilikuwa kali katika dunia yote.


Basi, wana wa Israeli wakafika Misri wakiwa kati ya wanunuzi wengine, maana hata katika inchi ya Kanana kulikuwa njaa.


Kisha njaa ikazidi kuwa kali katika inchi ya Kanana.


Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”


Ira wa muji Yairi alikuwa vilevile kuhani wa Daudi.


Wao wakamwambia mufalme: “Saulo alikusudia kutuua sisi na kutuangamiza kusipate kubakia mutu yeyote wetu popote katika eneo lolote la Israeli.


Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.


Basi, Daudi alimwuliza Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia Daudi: “Kwenda, maana hakika nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”


Daudi alipomwomba Yawe shauri, Yawe alimwambia: “Usiwashambulie kutoka hapa unapokuwa, lakini zunguka nyuma yao na kuwashambulia kutokea mbele ya miti ya miforosadi.


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.


Matokeo yake ilikuwa njaa kali katika muji wa Samaria. Kichwa cha punda kilinunuliwa kwa vikoroti makumi tatu vya feza, na grama mia moja za mavi ya njiwa zilinunuliwa kwa vikoroti vitano vya feza.


Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”


Nitamwambia Mungu: Usinitendee sawa na mwenye makosa. Unijulishe sababu ya kugombana nami.


Moyo wangu unaniambia: “Kuja umutafute Mungu!” Basi, ninakutafuta, ee Yawe.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.


Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.


Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu juu ya vile vitu vilivyotolewa viangamizwe maana Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi, wa ukoo wa Zera, wa kabila la Yuda, alitwaa vimoja kati ya vitu vilivyoamriwa viteketezwe. Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli.


Tutawaacha waishi, kusudi tusipate kuazibiwa kwa sababu ya kiapo tulichofanya.


Hapo zamani, wakati waamuzi walipokuwa wanatawala Waisraeli, kulitokea njaa katika inchi. Mutu mumoja kutoka Betelehemu katika Yuda pamoja na muke wake na watoto wao wanaume wawili walikwenda kuishi kwa muda katika inchi ya Moabu kwa kuishi kama wageni.


Wakamwuliza Mungu tena: “Kuna mutu zaidi anayekuja?” Yawe akawajibu: “Anajificha kwenye mizigo.”


Wakaaji wa Keila watanitia katika mikono ya Saulo? Saulo atakuja kweli kama nilivyosikia mimi mutumishi wako? Ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba unijibu mimi mutumishi wako.” Yawe akamujibu: “Saulo atakuja.”


Basi, Daudi akamwomba Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini hawa?” Yawe akamujibu: “Ndiyo, kwenda kuwashambulia Wafilistini na kuuokoa muji wa Keila.”


Daudi akamwomba tena Yawe shauri, naye Yawe akamwambia: “Simama uende Keila maana nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ