Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Ulivyosema si kweli! Lakini mutu mumoja kutoka sehemu ya milima ya Efuraimu anayeitwa Seba mwana wa Bikiri anataka kumwasi mufalme Daudi. Mumutoe kwangu nami nitaondoka katika muji wenu.” Yule mwanamuke akamwambia Yoabu: “Kichwa chake kitarushwa kwako kupitia juu ya ukuta.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:21
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Kwa hiyo, watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi, wakamufuata Seba mwana wa Bikiri. Lakini watu wa Yuda walimufuata mufalme Daudi kwa uaminifu toka muto Yordani mpaka Yerusalema.


Yoabu akamujibu: “Hata kidogo katika maisha yangu! Sina nia ya kuangamiza wala kuharibu.


Abisayi mwana wa Zeruya na ndugu ya Yoabu alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia sifa pamoja na wale mashujaa watatu.


Yeroboamu mwana wa Nebati Mwefuraimu wa muji wa Zereda, mutumishi wa Solomono, ambaye mama yake mujane aliitwa Zerua, naye alimwasi mufalme.


Basi, barua ilipowafikia, waliwatwaa hao wana wa mufalme na kuwakata vichwa wote makumi saba. Waliweka vichwa vyao katika vikapu na kumupelekea Yehu kule Yezereheli.


Gehazi akajibu: “Mambo yote ni sawa lakini tu bwana wangu amenituma nikuambie kwamba sasa hivi amepokea watu wawili wa kundi la manabii katika inchi ya milima ya Efuraimu, naye angependa uwape vikoroti elfu tatu vya feza na nguo mbili ya sikukuu.”


Sauti kutoka Dani inatoa tangazo; inatangaza hasara kutoka vilima vya Efuraimu.


Nitawarudisha Waisraeli katika inchi yao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mulima Karmeli na Basani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efuraimu na Gileadi.


Naye Eleazari mwana wa Haruni, akakufa na kuzikwa Gibea, muji ambao mwana wake Finehasi alikuwa amepewa katika inchi ya milima ya Efuraimu.


Wakamuzika katika sehemu aliyogawanyiwa ikuwe yake kule Timunati-Heresi, katika inchi ya milima ya Efuraimu upande wa kaskazini wa mulima Gasi.


Gideoni akatuma wajumbe katika inchi yote ya milima ya Efuraimu watangaze: “Muteremuke kwa kuwafuata Wamidiani na kuwazuia kwa kuteka vijito na muto Yordani mpaka Beti-Bara.” Basi, wanaume wote wa Efuraimu wakakuja na kuuteka muto Yordani mpaka Beti-Bara.


Waisraeli walipoona kwamba Abimeleki amekufa, wakaondoka na kurudi kila mumoja kwake.


Daudi akaanza kufazaika ndani ya moyo kwa sababu alikata pindo la nguo ya Saulo kwa siri.


Lakini Daudi akamwambia Abisai: “Usimwangamize; maana nani anaweza kunyoosha mukono wake juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe, naye asiazibiwe?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ