2 Samweli 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20022 Kwa hiyo, watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi, wakamufuata Seba mwana wa Bikiri. Lakini watu wa Yuda walimufuata mufalme Daudi kwa uaminifu toka muto Yordani mpaka Yerusalema. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”
Nyuma, Daudi alifika katika nyumba yake kule Yerusalema. Mufalme aliwatwaa wahabara wake kumi ambao alikuwa amewaacha kwa kuangalia nyumba yake, akawaweka kwenye nyumba moja wapate kulindwa, akawatunza vizuri, lakini hakulala nao. Kwa hiyo wahabara hao wakakuwa wakifungwa mpaka siku za kufa kwao, wakaishi kama vile walikuwa wajane.