Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa hiyo, watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi, wakamufuata Seba mwana wa Bikiri. Lakini watu wa Yuda walimufuata mufalme Daudi kwa uaminifu toka muto Yordani mpaka Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:2
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Daudi aliivuta mioyo ya watu wote wa Yuda kama mutu mumoja. Halafu, wakamupelekea ujumbe kusema: “Rudi kwako, wewe na watumishi wako wote.”


Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Ulivyosema si kweli! Lakini mutu mumoja kutoka sehemu ya milima ya Efuraimu anayeitwa Seba mwana wa Bikiri anataka kumwasi mufalme Daudi. Mumutoe kwangu nami nitaondoka katika muji wenu.” Yule mwanamuke akamwambia Yoabu: “Kichwa chake kitarushwa kwako kupitia juu ya ukuta.”


Nyuma, Daudi alifika katika nyumba yake kule Yerusalema. Mufalme aliwatwaa wahabara wake kumi ambao alikuwa amewaacha kwa kuangalia nyumba yake, akawaweka kwenye nyumba moja wapate kulindwa, akawatunza vizuri, lakini hakulala nao. Kwa hiyo wahabara hao wakakuwa wakifungwa mpaka siku za kufa kwao, wakaishi kama vile walikuwa wajane.


Watu wote wa Israeli walipopata habari kwamba Yeroboamu alikuwa amerudi kutoka Misri, walimwita katika mukutano, wakamuweka kuwa mufalme wa Israeli yote. Hakuna kabila lingine lililojiunga na ukoo wa Daudi isipokuwa tu kabila la Yuda.


Lakini Rehoboamu alitawala watu wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda.


Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote; mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu. Yeye ndiye kimbilio letu.


Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ