Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Mimi ni mumoja wa wale wanaopenda amani na uaminifu katika Israeli. Sasa wewe unakusudia kuuharibu muji ambao ni sawa vile katika Israeli. Kwa nini sasa unataka kuuangamiza muji unaokuwa mali ya Yawe?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:19
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Abrahamu akamukaribia Yawe, akamwuliza: “Ni kweli utawaangamiza watu wa haki pamoja na waovu?


Maana mufalme atanisikiliza na kuniokoa toka katika mikono ya mutu ambaye anataka kuniangamiza mimi pamoja na mwana wangu kutoka urizi wa Mungu.


Kisha akasema, “Mupelekee Daudi habari upesi kwamba asilale usiku kwenye vivuko katika jangwa, lakini lazima avuke muto Yordani kusudi asikamatwe na kuuawa, yeye pamoja na watu wake wote.”


Yule mwanamuke akamwambia: “Zamani watu walikuwa wakisema: ‘Muache waombe shauri kutoka muji wa Abeli’. Ndivyo watu walivyoweza kutatua matatizo.


Yoabu akamujibu: “Hata kidogo katika maisha yangu! Sina nia ya kuangamiza wala kuharibu.


Daudi akawauliza Wagibeoni: “Niwatendee nini? Nitalipa namna gani maovu muliyotendewa kusudi mupate kuibariki inchi hii na watu wa Yawe?”


Kwa sababu, ee Bwana wetu Yawe, uliwatenga na watu wa mataifa mengine katika dunia, kusudi wakuwe mali yako, kama ulivyotangaza kwa njia ya Musa, mutumishi wako, wakati ule ulipowatoa babu zetu katika inchi ya Misri.”


kusudi niweze kuona uheri wa wachaguliwa wako, nipate kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuona utukufu pamoja na watu wako.


hakika tungalimezwa tukikuwa wazima, wakati hasira yao ilipowaka juu yetu.


Heri taifa ambalo Mungu wake ni Yawe; heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!


Alimutoa katika kazi ya kuchunga kondoo na wana-kondoo, akuwe na madaraka ya kuchunga watu wa Yakobo taifa lake, achunge Israeli, watu wa pekee wa Mungu.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Waadui zako wote wanakuzomea, wanakupigia muunzi na kukusagia meno, nao wanasema: Tumemwangamiza! Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu sasa imefika na tumeiona!


Yawe ameharibu bila huruma makao yote ya wazao wa Yakobo. Kwa kasirani yake amevibomoa vikingio vya watu wa Yuda. Ametupa chini na kuchafua ufalme wao na watawala wake.


Yawe amekuwa kama adui, ameangamiza watu wa Israeli; ameharibu nyumba zake kubwa zote, amevibomoa vikingio vyake. Amewazidishia watu wa Yuda kilio na maombolezo.


na kuwameza watu hao, jamaa zao, pamoja na wafuasi wote wa Kora na mali zao zote.


Wakati huo udongo ukafunguka ikawameza, wakakufa pamoja na Kora na wafuasi wake moto ulipoangamiza watu mia mbili makumi tano; wakakuwa onyo kwa watu.


Na wakati mwili huu wa kuharibika utakapovaa ule wa kutoharibika, nao mwili wa kufa utakapovaa ule wa kutokufa, halafu Maandiko Matakatifu haya yatatimia: “Kifo kimekomeshwa; kimeshindwa kabisa.”


Hakika kwa wakati wowote tungali tunaishi katika makao haya ya dunia, tunaugua kwa kulemewa. Si kwa sababu tunataka kuondolewa mwili wa dunia, lakini tunataka kuvaa mwili wa mbinguni, kusudi uzima wa milele upate kubadilisha miili yetu inayokuwa ya kufa.


“Munapokaribia muji kwa kuushambulia, kwanza muwape wakaaji wake masharti ya amani.


lakini alijiwekea watu wa Yakobo kuwa wake, hao alijichagulia kuwa mali yake.


Inafaa kuombea wafalme na watu wenye mamlaka kusudi tupate kuishi katika ukimya na amani katika kushikamana na ibada na katika mwenendo safi.


Walimaji walitoweka, walitoweka katika Israeli, mpaka nilipotokea mimi Debora, mimi ninayekuwa mama wa Israeli.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ