18 Yule mwanamuke akamwambia: “Zamani watu walikuwa wakisema: ‘Muache waombe shauri kutoka muji wa Abeli’. Ndivyo watu walivyoweza kutatua matatizo.
Yoabu akaenda karibu naye, huyo mwanamuke akamwambia: “Wewe ndiwe Yoabu?” Yoabu akasema: “Ndiyo! Ni mimi.” Yule mwanamuke akamwambia: “Unisikilize mimi mujakazi wako.” Yoabu akamwambia: “Ninasikiliza.”
Mimi ni mumoja wa wale wanaopenda amani na uaminifu katika Israeli. Sasa wewe unakusudia kuuharibu muji ambao ni sawa vile katika Israeli. Kwa nini sasa unataka kuuangamiza muji unaokuwa mali ya Yawe?”