Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakaenda kumuzunguka Seba akiwa katika muji ule wa Abeli wa Beti-Maka. Walilundika udongo kwa kuzunguka muji, na makimbilio. Halafu wakaanza kuubomoa ukuta kwa kuuangusha chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:15
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Seba alipita katika makabila yote ya Israeli mpaka katika muji wa Abeli wa Beti-Maka. Watu wote wa ukoo wa Bikiri wakakusanyika na kumufuata.


Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubaliana na mufalme Asa, akawatuma majemadari wake na waaskari wake kwenda kuishambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji Iyoni, Dani, Abeli-Beti-Maka, Kineroti yote, na inchi yote ya Nafutali.


Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


“Yawe anasema hivi juu ya mufalme wa Asuria: Hataingia katika muji huu, wala kuupiga mushale, wala kuingia akishika ngao, wala hatalundika udongo kandokando yake apate kuubomoa.


Kulikuwa muji mumoja mudogo wenye wakaaji wachache. Mufalme mumoja mwenye nguvu akafika, akauzunguka na kujitayarisha kuushambulia.


Yawe anasema hivi juu ya mufalme wa Asuria: Hataingia katika muji huu, wala kuupiga mushale, wala kuingia akishika ngao, wala hatalundika udongo kandokando yake apate kuubomoa.


Angalia, Wakaldea wamechimba mifereji kuuzunguka muji; wanauzunguka kusudi wapate kuuteka; wanaushambulia. Vita, njaa na magonjwa vitaufanya muji utekwe na watu hao. Kweli mambo uliyotabiri yametokea. Unaona mwenyewe.


Maana Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda zilizobomolewa kwa sababu ya vita.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.


Onyesha kwamba muji ule umeshambuliwa. Utaujengea nafasi za kupandia juu ya kuta zake. Kandokando yake uweke makambi ya waaskari, na gongo ya kubomoa kuta.


Kwa maana siku zitakufikia wakati waadui zako watakapokuzunguka kwa vita, watakapojenga ukuta wa kujikingia pembeni yako, na kukusonga pande zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ