Watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakaenda kumuzunguka Seba akiwa katika muji ule wa Abeli wa Beti-Maka. Walilundika udongo kwa kuzunguka muji, na makimbilio. Halafu wakaanza kuubomoa ukuta kwa kuuangusha chini.
Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubaliana na mufalme Asa, akawatuma majemadari wake na waaskari wake kwenda kuishambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji Iyoni, Dani, Abeli-Beti-Maka, Kineroti yote, na inchi yote ya Nafutali.
Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.
Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubali pendekezo la mufalme Asa. Akawatuma majemadari wake na majeshi yake kwenda kushambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji ya Iyoni, Dani, Abeli-Maimu, na miji yote ya Nafutali iliyokuwa na hazina.