Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Amasa alipoondolewa kwenye barabara kubwa, watu wote sasa waliendelea kumufuata Yoabu kwa kumufuatilia Seba mwana wa Bikiri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:13
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Mutu mumoja wa Yoabu akakuja akasimama karibu na mwili wa Amasa, akasema: “Yeyote anayemupenda Yoabu na yeyote anayemupenda Daudi, amufuate Yoabu!”


Seba alipita katika makabila yote ya Israeli mpaka katika muji wa Abeli wa Beti-Maka. Watu wote wa ukoo wa Bikiri wakakusanyika na kumufuata.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma majemadari wakubwa watatu pamoja na kundi kubwa la waaskari kutoka Lakisi kwenda kwa mufalme Hezekia kule Yerusalema. Walisafiri na kufika Yerusalema. Nao walipofika waliingia na kusimama karibu na mufereji wa kisima kinachokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea kiwanja cha mufuaji wa nguo.


Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma jemadari kutoka Lakisi na kundi kubwa kumwendea mufalme Hezekia. Jemadari yule alisimama karibu na mufereji wa birika linalokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea shamba la wafuaji wa nguo.


Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Yawe akamwambia Isaya: Uende pamoja na mwana wako anayeitwa Watakaobaki-Watarudi, kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.


Weka kitambulisho katika njia zako, simika nguzo za kukuongoza, ukumbuke vema ile njia kubwa, barabara uliyopita ndani yake ukienda. Ewe Israeli rudi, rudi kwa nyumba katika miji yako.


Waisraeli wakamwambia: Sisi tutafuata njia kubwa; kama sisi na mifugo yetu tukikunywa maji yenu, tutalipa. Tunachoomba tafazali uturuhusu tu, tupite kwa miguu wala hatutaki neno lolote lingine.


Wakafika Yeriko. Na wakati Yesu alipokuwa akitoka kule pamoja na wanafunzi wake na kundi kubwa la watu, mutu mumoja kipofu aliyeitwa Bartimayo mwana wa Timayo, alikuwa akiikaa pembeni ya njia akiombaomba.


Basi wakakumbuka kwamba sikukuu ya Yawe iliyofanyika kila mwaka kule Shilo, muji unaokuwa upande wa kaskazini wa Beteli, kwenye njia kubwa inayotoka Beteli kwenda Sekemu, ilikuwa inakaribia.


Wale ngombe walikwenda moja kwa moja kuelekea muji wa Beti-Semesi bila kupinda kushoto au kuume, walikuwa wanalia walipokuwa wanakwenda. Wale wafalme watano wa Wafilistini waliwafuata mpaka kwenye mupaka wa Beti-Semesi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ