Amasa alikuwa bado anagaagaa ndani ya damu yake katikati ya barabara kubwa. Kwa hiyo, kila mutu aliyepita pale, alipomwona, alisimama. Lakini yule mutu alipoona kwamba watu wote walikuja na kusimama pale, aliuondoa mwili wa Amasa ndani ya barabara, akaupeleka katika shamba na kuufunika kwa nguo.
Ulivyosema si kweli! Lakini mutu mumoja kutoka sehemu ya milima ya Efuraimu anayeitwa Seba mwana wa Bikiri anataka kumwasi mufalme Daudi. Mumutoe kwangu nami nitaondoka katika muji wenu.” Yule mwanamuke akamwambia Yoabu: “Kichwa chake kitarushwa kwako kupitia juu ya ukuta.”
Yehu akaangalia juu na kusema: “Ni nani anayekuwa upande wangu?” Wakubwa wawili au watatu wakatokeza vichwa vyao kwa kumwangalia kutoka kwenye dirisha,