Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 20:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini Amasa hakuona upanga uliokuwa katika mukono wa Yoabu. Basi, Yoabu akamuchoma Amasa upanga ndani ya tumbo, matumbotumbo yake yakatoka inje, akakufa. Yoabu hakumuchoma upanga mara mbili. Kisha, Yoabu na ndugu yake Abisayi wakaendelea kumufuatilia Seba mwana wa Bikiri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 20:10
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Kaina akasemezana na ndugu yake Abeli. Basi, walipokuwa katika shamba, Kaina akamushambulia ndugu yake Abeli, akamwua.


Lakini Asaeli alikataa. Kwa hiyo Abeneri akamupiga mukuki ndani ya tumbo kinyumenyume, na mukuki huo ukatokea katika mugongo wa Asaeli. Asaeli akaanguka chini na kufa pale pale. Watu wote waliofika pahali Asaeli alipokufia, walisimama kimya.


Yoabu akamwambia Amasa: “Habari gani ndugu yangu?” Yoabu akamushika Amasa kwenye kidevu kwa mukono wa kuume sawa vile anataka kumubusu.


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Walikuwa wa kabila la Benjamina kama vile Saulo alivyokuwa. Walikuwa wapiga upinde hodari, na warusha mawe hodari kwa kutumia mikono yote, wa kuume na wa kushoto. Haya ndiyo majina yao:


Isimaeli mwana wa Netania pamoja na wale watu kumi, wakasimama na kumushambulia kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, wakamwua. Gedalia ndiye aliyekuwa amesimikwa na mufalme wa Babeli kuwa mutawala wa inchi.


Vilevile, kama mutu anamuchukia mwenzake halafu, akimusukuma au kumutupia kitu kwa kumuvizia,


Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.


Ehudu akauchomoa upanga wake kwa mukono wake wa kushoto kutoka paja lake la kuume, akamuchoma nao katika tumbo lake.


Abisai akamwambia Daudi: “Leo Mungu amemutia adui yako katika mikono yako. Basi, uniache nimushindilie katika udongo kwa pigo moja tu la mukuki. Sitamupiga mara mbili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ