Wewe ulikuja huku juzijuzi tu. Nikufanye mutu wa kutangatanga pamoja nasi, nikijua kwamba sijui hata kule ninakokwenda? Rudi pamoja na wandugu zako. Naye Yawe akuonyeshe wema na uaminifu.”
Alikwenda na kuitwaa mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kwa wakaaji wa Yabeshi-Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka kule Beti-Sani, ambako Wafilistini walikuwa wamemutundika Saulo na Yonatani siku ile walipomwua Saulo kwenye mulima Gilboa.
Wakataka kujua kama kulikuwa kikundi chochote cha makabila ya Israeli ambacho hakikuhuzuria mukutano mbele ya Yawe kule Mispa. Wakagundua kwamba hakuna mutu yeyote kutoka Yabesi-Gileadi aliyekuja kwenye mukutano ule.
Naomi akawaambia hao wakwe zake wawili: “Murudi kila mumoja kwa mama yake. Ninaomba Yawe awatendee mema kama vile mulivyonitendea mema mimi na wale watu wangu waliokufa.
Basi, Naomi akamwambia mukwe wake: “Yawe amubariki Boazi! Mungu anatimiza siku zote ahadi zake kwa wanaokuwa wazima na waliokufa.” Kisha akaendelea kusema: “Huyo mutu ni ndugu yetu wa karibu na ni mumoja wa wale wenye mapaswa ya kututunza.”
Boazi akasema: “Yawe akubariki, kwa maana kwa yote unayofanya unaonyesha heshima zaidi kuliko uliyoyafanya pale mbele, kwa maana haukuwatafuta vijana wamasikini au tajiri wakuoe.
Mufalme Nahasi wa Waamoni, alikwenda na kuushambulia muji wa Yabesi-Gileadi. Wakaaji wa muji wa Yabesi-Gileadi wakamwambia Nahasi: “Fanya mapatano nasi, nasi tutakutumikia.”
Wakawaambia wale wajumbe waliorudi kutoka Yabesi: “Muwaambie wakaaji wa Yabesi-Gileadi hivi: kesho, wakati jua linapokuwa kali, mutakuwa mumekombolewa.” Watu wa Yabesi walipopata habari hizo walifurahi sana.