Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 2:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Lakini Asaeli alikataa. Kwa hiyo Abeneri akamupiga mukuki ndani ya tumbo kinyumenyume, na mukuki huo ukatokea katika mugongo wa Asaeli. Asaeli akaanguka chini na kufa pale pale. Watu wote waliofika pahali Asaeli alipokufia, walisimama kimya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 2:23
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yoabu na Abisayi walimufuatilia Abeneri. Jua lilipokuwa linatua wakafika kwenye mulima Ama, unaokuwa upande wa mashariki ya Gia, katika barabara inayokwenda katika jangwa la Gibeoni.


Lakini Amasa hakuona upanga uliokuwa katika mukono wa Yoabu. Basi, Yoabu akamuchoma Amasa upanga ndani ya tumbo, matumbotumbo yake yakatoka inje, akakufa. Yoabu hakumuchoma upanga mara mbili. Kisha, Yoabu na ndugu yake Abisayi wakaendelea kumufuatilia Seba mwana wa Bikiri.


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Yoabu na ndugu yake Abisayi walimwua Abeneri kwa sababu alikuwa amemwua ndugu yao Asaeli wakati wa vita kule Gibeoni.


Waliingia ndani ya nyumba wakijifanya sawa vile wanataka kukamata ngano, walimukuta Isiboseti amelala juu ya kitanda chake ndani ya chumba chake cha kulala, wakamuchoma mukuki katika tumbo. Kisha kumwua hivyo hao wandugu wawili walimukata kichwa wakatoroka wakikibeba. Walipitia njia ya Araba, wakasafiri usiku kucha.


Kisha mufalme na watu wake walikwenda Yerusalema kuwashambulia Wayebusi waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo. Lakini wao wakamwambia: “Hautaingia ndani ya muji huu, maana vipofu na vilema watakufukuza.” Walimwambia hivyo maana walifikiri kwamba Daudi asingeweza kuingia katika muji ule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ