2 Samweli 2:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200223 Lakini Asaeli alikataa. Kwa hiyo Abeneri akamupiga mukuki ndani ya tumbo kinyumenyume, na mukuki huo ukatokea katika mugongo wa Asaeli. Asaeli akaanguka chini na kufa pale pale. Watu wote waliofika pahali Asaeli alipokufia, walisimama kimya. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Waliingia ndani ya nyumba wakijifanya sawa vile wanataka kukamata ngano, walimukuta Isiboseti amelala juu ya kitanda chake ndani ya chumba chake cha kulala, wakamuchoma mukuki katika tumbo. Kisha kumwua hivyo hao wandugu wawili walimukata kichwa wakatoroka wakikibeba. Walipitia njia ya Araba, wakasafiri usiku kucha.