Halafu vijana makumi mbili na ine wakatolewa: upande wa kabila la Benjamina na Isiboseti mwana wa Saulo, vijana kumi na wawili; na upande wa Daudi, vijana kumi na wawili.
Kila mumoja alimukamata adui yake kwenye kichwa, na kumuchoma upanga katika ubavu. Hivyo wote wawili wakaanguka chini, wamekufa. Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Shamba la Mapanga. Pahali pale pako kule Gibeoni.