Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.
Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema: “Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni, wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”
Habari hizo zilisababisha hofu kubwa kule Yerusalema kwa sababu muji wa Gibeoni ulikuwa mukubwa sana kati ya miji ya kifalme. Muji huu ulikuwa vilevile mukubwa kuliko Ai na wanaume wake wote walikuwa waaskari hodari sana.