Tena Abusaloma ambaye tulimupakaa mafuta akuwe mufalme wetu, sasa ameuawa katika vita. Sasa, kwa nini hatuzungumuzii juu ya kumurudisha mufalme Daudi?”
Mufalme Daudi akatuma ujumbe kwa makuhani Zadoki na Abiatari: “Muwaambie wazee wa Yuda: ‘Kwa nini ninyi ndio mutakuwa wa mwisho kumurudisha mufalme katika nyumba yake? Maneno yote Waisraeli waliyosema yamenifikia mimi mufalme.
Watu wa kabila la Efuraimu wakakusanyika, wakavuka muto Yordani wakafika kule Safoni. Kisha wakamwambia Yefuta: “Kwa nini haukutuita tuende pamoja nawe kupigana na Waamoni? Sasa tutaichoma nyumba yako nawe mwenyewe ndani yake.”
Watu wa kabila la Efuraimu wakamwuliza Gideoni: “Kwa nini umetutendea hivyo? Kwa nini haukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakamugombeza kwa ukali.