Watu wote walikuwa wanabishana wao kwa wao katika makabila yote ya Israeli, wakisema: “Mufalme Daudi alitukomboa toka mikono ya waadui zetu, alituokoa toka mikono ya Wafilistini. Lakini sasa ameikimbia inchi, akimukimbia Abusaloma.
Kisha, mufalme akatoka, akaenda, akaikaa kwenye nafasi yake karibu na mulango. Watu wote walipoambiwa kwamba mufalme yuko kwenye mulango, wote walimwendea. Wakati ule, watu wote wa Israeli walikuwa wamekimbia, kila mumoja kwake.
Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”