Mufalme akamujibu: “Sivyo, mwana wangu, tusiende wote, kusudi tusikuwe muzigo kwako.” Ingawa Abusaloma alizidi kumusihi baba yake aende, lakini mufalme alikataa, lakini alimupa baraka zake.
Kwa hiyo Yoabu akaenda na kumwelezea mufalme maneno hayo yote, naye akamwita Abusaloma. Abusaloma akaingia kwa mufalme, akaanguka uso mpaka chini mbele ya mufalme. Na mufalme akamubusu Abusaloma.
Ninakuomba uniruhusu mimi mutumishi wako, nikufie katika muji wangu, karibu na kaburi la baba yangu na mama yangu. Lakini huyu mutumishi wako Kimuhamu, umuruhusu aende pamoja nawe bwana wangu mufalme, na umutendee yeye lolote unaloona ni zuri.”
Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”
Halafu, Elisha akawaacha ngombe wake, akamufuata Elia mbio na kumwambia: “Uniruhusu kwanza niende kumupa baba yangu na mama yangu busu la kwa heri, kisha nikufuate.” Elia akamujibu: “Kwenda! Ni nini niliyokutendea?”
Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,