Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 19:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Mimi mutumishi wako nitakwenda nawe mwendo mufupi ngambo ya Yordani. Kwa nini, mufalme anilipe zawadi kubwa hivyo?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 19:37
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

lakini unilalishe pamoja na babu zangu. Unitwae kutoka Misri na kunizika katika makaburi yao.” Yosefu akamujibu: “Nitafanya kama ulivyosema.”


Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.


wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.


Mimi leo nina umri wa miaka makumi nane. Niko na uwezo wa kutambua yanayokuwa mazuri na yale yasiyokuwa mazuri? Mimi mutumishi wako ninaweza tena kutambua onjo ya kile ninachokula au kunywa? Nitaweza tena kutambua uzuri wa sauti za waimbaji wanaume au wanawake? Kwa nini mimi mutumishi wako nikuwe muzigo wa zaidi kwako bwana wangu mufalme?


Ninakuomba uniruhusu mimi mutumishi wako, nikufie katika muji wangu, karibu na kaburi la baba yangu na mama yangu. Lakini huyu mutumishi wako Kimuhamu, umuruhusu aende pamoja nawe bwana wangu mufalme, na umutendee yeye lolote unaloona ni zuri.”


Halafu watu wote wakavuka muto Yordani na mufalme naye akavuka. Mufalme akamubusu na kumubariki Barzilayi, na Barzilayi akarudi kwake.


Kwa pahali pake, umerudi hapa, ukakula chakula na kunywa maji pahali hapa ambapo uliambiwa usikule chakula wala kunywa maji. Basi, mwili wako hautazikwa kwenye kaburi la babu zako.’ ”


“Lakini uwatendee mema wana wa Barzilayi, yule Mugileadi, wakuwe kati ya wale wanaokula kwenye meza yako, kwa sababu walinitendea mema wakati nilipomukimbia ndugu yako Abusaloma.


Basi, wakajiendea, wakakaa huko Geruti–Kimuhamu karibu na Betelehemu. Wakikusudia kuingia katika inchi ya Misri, kwa sababu


Kwa maana, mimi sasa niko tayari kutolewa kama sadaka, na wakati wa kufa kwangu umekaribia.


“Sasa, wakati wangu wa kufa kama inavyokuwa kawaida ya wanadamu wote umekaribia. Lakini ninyi wote munajua wazi ndani ya mioyo na roho zenu kwamba katika mambo yote mema ambayo Yawe, Mungu wenu aliwaahidi, hakuna hata moja ambalo halikutimia. Yote yametimia kama vile alivyoahidi.


Kwa maana ninajua kwamba ninakaribia kuacha mwili huu unaokuwa wa kufa kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha waziwazi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ