2 Samweli 19:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
32 Barzilayi wa Gileadi alikuwa amefika kutoka Rogelimu. Alikuwa amekwenda pamoja na mufalme kwenye muto Yordani kwa kumusindikiza mpaka ngambo ya muto.
Basi, Yosefu akakufa kule Misri, akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi. Nao wakapakaa mwili wake dawa kusudi usioze, wakauweka katika sanduku kule Misri.
Barzilayi alikuwa muzee sana, mwenye umri wa miaka makumi nane. Naye Barzilayi alikuwa amemutunza mufalme alipokaa kule Mahanaimu, kwa sababu alikuwa tajiri sana.
Menahemu alipata feza hiyo kwa kuwalazimisha watajiri wa Israeli kutoa muchango wa vikoroti makumi tano vya feza kila mumoja. Halafu Puli hakukaa Israeli lakini akarudi katika inchi yake.
Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.
Kulikuwa mutu mumoja kule katika muji wa Maoni ambaye alikuwa na biashara ya kondoo katika muji wa Karmeli. Kule Karmeli alifuga kondoo wake na kuwakata manyoya. Alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja.