Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 19:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Sasa, amenisingizia kwako, ee bwana wangu mufalme. Lakini wewe, bwana wangu mufalme, uko kama malaika wa Mungu. Fanya sawa unavyotaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 19:28
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,


Nami mujakazi wako nilifikiri hivi: ‘Neno la bwana wangu mufalme litanipa amani ndani ya moyo, maana wewe bwana wangu mufalme ni kama malaika wa Mungu katika kupambanua mazuri na mabaya.’ Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe.”


Yoabu alifanya hivyo kwa kubadilisha mambo. Lakini, wewe bwana wangu, una hekima kama ya malaika wa Mungu hata unaweza kujua mambo yote yanayokuwa katika dunia.”


Lakini ikiwa Yawe hapendezwi nami basi, mimi niko tayari; na anitendee sawa vile anavyotaka.”


Mufalme akamwuliza: “Mwana wa bwana wako yuko wapi?” Siba akamwambia mufalme: “Yeye amebaki Yerusalema kwa sababu anazani kwamba watu wa Israeli watamurudishia ufalme wa Saulo babu yake.”


Maana, jamaa yote ya babu yangu walikuwa watu ambao wamestahili kuuawa mbele yako, bwana wangu mufalme. Lakini uliniweka mimi mutumishi wako kati ya wale wanaokula kwenye meza yako. Nina haki yoyote zaidi hata nikulilie mufalme?”


Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.


Kwa hiyo, Mefiboseti aliyekuwa kilema wa miguu yake yote akakuwa anaishi katika Yerusalema, na kupata chakula chake kwenye meza ya mufalme siku zote.


Miaka saba ilipokwisha, alitoka katika inchi ya Wafilistini akarudi Israeli na kwenda kwa mufalme kuomba arudishiwe nyumba yake na shamba lake.


Ulilotenda si jambo zuri. Kama vile Yawe anavyoishi, unastahili kufa, maana haukumulinda bwana wako, ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Sasa angalia, mukuki wa mufalme na ule mufuko wa maji uliokuwa karibu na kichwa chake kama vipo!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ