Kisha, Daudi akasimama, akaoga, akajipakaa mafuta na kubadilisha nguo zake. Halafu akaenda katika nyumba ya Yawe na kuabudu. Kisha akarudi kwake, akaamuru wamuletee chakula, naye akakula.
Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.
Mufalme akamwuliza: “Mwana wa bwana wako yuko wapi?” Siba akamwambia mufalme: “Yeye amebaki Yerusalema kwa sababu anazani kwamba watu wa Israeli watamurudishia ufalme wa Saulo babu yake.”
Kisha, Siba akamwambia mufalme: “Mimi mutumishi wako, nitafanya yote kulingana na amri yako.” Basi, Mefiboseti akakuwa anapata chakula chake kwenye meza ya Daudi, kama vile mumoja wa watoto wa mufalme.
Vilevile, kuko Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina wa muji wa Bahurimu, ambaye aliniapiza na kunilaani vikali nilipokwenda kule Mahanaimu; lakini alipokuja kunipokea kwenye muto Yordani, nilimwapia kwa jina la Yawe nikimwambia: ‘Sitakuua kwa upanga.’
Watu wa Diboni wamepanda katika hekalu pahali pa juu kwa kuomboleza, watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba; vichwa vyote vimenyolewa upaa, ndevu zao zote zimekatwa kabisa.
mbele hata mutu yeyote hajajua habari hizo, kulifika watu makumi nane kutoka Sekemu, Shilo na Samaria. Walikuwa wamenyoa ndevu zao na wamevaa nguo zilizotatuka na miili yao imechanjwachanjwa. Walileta sadaka ya ngano na ubani vitolewe katika nyumba ya Yawe.
“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.
Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.