2 Yoabu alipata habari kwamba mufalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Abusaloma.
Yoabu mwana wa Zeruya alitambua kwamba moyo wa Daudi ulikuwa unamwelekea Abusaloma tu.
Hapo mufalme alishikwa na huzuni kubwa, akapanda kwenye chumba kilichokuwa juu ya mulango na kulia. Alipokuwa anapanda, alilia akisema: “Mwana wangu Abusaloma, mwana wangu Abusaloma! Ingekuwa heri ningalikufa pahali pako! Ole, Abusaloma mwana wangu! Mwana wangu!”
Ushindi wa siku hiyo uligeuzwa kuwa maombolezo kwa watu wote, waliposikia kwamba mufalme anamwombolezea Abusaloma.
Uso wa mufalme ukiangaa, kuna uzima; kupendwa naye ni kama wingu la mvua kwa shamba.
Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.