Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 19:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Basi, wakavuka kwenye kivuko kwa kuisindikiza jamaa ya mufalme na kumufanyia mufalme yote aliyoyapenda. Simei mwana wa Gera akakuja, akajitupa mbele ya mufalme, akainama uso mpaka chini, wakati mufalme alipokuwa karibu kuvuka muto Yordani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 19:19
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kaka yake, Abusaloma, alipomwona, alimwuliza: “Kaka yako Amunoni amelala nawe? Tulia dada yangu. Yeye ni kaka yako. Usichunge jambo hilo ndani ya moyo wako.” Halafu, Tamari aliishi katika nyumba ya Abusaloma akiwa na huzuni na mwenye kutupiliwa.


Kwa hiyo, bwana wangu, usifikiri ndani ya moyo wako kwamba watoto wako wote wamekufa. Ni Amunoni pekee ndiye aliyeuawa.”


Simei alikwenda pamoja na watu wa kabila la Benjamina elfu moja. Siba mutumishi wa jamaa ya Saulo, pamoja na watoto wake kumi na watumishi makumi mbili, walikwenda haraka kwenye muto Yordani kumutangulia mufalme Daudi.


Heri mutu ambaye Yawe hamuhesabii kosa, mutu ambaye hana udanganyifu ndani ya moyo wake.


Usituazibu kwa sababu ya makosa ya babu zetu. Huruma yako itufikie haraka, maana tumegandamizwa sana!


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Hapo, Haruni akamwambia Musa: Ewe bwana wangu, tumetenda mambo ya kipumbafu na kufanya zambi. Lakini usituazibu!


Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Leo, sio mara ya kwanza kumwomba Mungu shauri kwa ajili yake. Mufalme, usiniwazie mimi wala mutu yeyote katika jamaa ya baba yangu juu ya mabaya yale. Mimi mutumishi wako, sijui neno lolote, likuwe kubwa au dogo juu ya jambo hilo.”


Usimwangalie Nabali ambaye ni mutu mubaya. Maana jina lake la Nabali linamustahili. Yeye anaitwa Nabali; na kweli yeye ni mutu mupumbafu. Bwana wangu, wale vijana wako ulipowatuma, mimi mujakazi wako sikuwaona.


Halafu Saulo akajibu: “Mimi nimefanya makosa. Rudi mwana wangu Daudi. Sitakuzuru tena kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa ya bei kali mbele yako. Mimi nimekuwa mupumbafu na nimekosa vibaya sana.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ