Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 19:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina, kutoka Bahurimu, alifanya haraka kwenda pamoja na watu wengine kwa kumupokea mufalme Daudi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 19:17
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.


Simei alikwenda pamoja na watu wa kabila la Benjamina elfu moja. Siba mutumishi wa jamaa ya Saulo, pamoja na watoto wake kumi na watumishi makumi mbili, walikwenda haraka kwenye muto Yordani kumutangulia mufalme Daudi.


Lakini Paltieli akaenda pamoja na muke wake akiwa analia njia yote mpaka kule Bahurimu. Abeneri akamwambia Paltieli: “Rudia kwako.” Naye akarudi.


Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.


Kulikuwa mutumishi wa jamaa ya Saulo aliyeitwa Siba. Siba aliitwa kwenda kwa Daudi. Mufalme Daudi alimwuliza: “Wewe ndiwe Siba?” Naye akamujibu: “Ndiyo, mimi mutumishi wako ndiye.”


Vilevile, kuko Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina wa muji wa Bahurimu, ambaye aliniapiza na kunilaani vikali nilipokwenda kule Mahanaimu; lakini alipokuja kunipokea kwenye muto Yordani, nilimwapia kwa jina la Yawe nikimwambia: ‘Sitakuua kwa upanga.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ