Basi, hivi ndivyo Abusaloma alivyowatendea Waisraeli wote waliokuja kutafuta uamuzi wa mufalme. Kwa kufanya hivyo, Abusaloma aliiteka mioyo ya Waisraeli.
Kisha Abeneri akamwita Yoabu: “Tutapigana siku zote? Hauoni kwamba mwisho utakuwa muchungu? Utaendelea kwa muda gani bila kuwashawishi watu wako kuacha kuwafuatilia wandugu zao?”
Peka, mwana wa Remalia akawaua watu wengi sana. Aliua waaskari mashujaa wa Yuda elfu mia moja na makumi mbili katika siku moja. Ilitokea vile kwa sababu walimwacha Yawe, Mungu wa babu zao.