2 Samweli 18:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Mufalme akawaambia: “Nitafanya sawa vile munavyoona kuwa vizuri.” Kwa hiyo, mufalme akasimama pembeni ya mulango, nao waaskari wake wakipita: mamia na maelfu.
Daudi aliwahesabu watu waliokuwa pamoja naye, akawagawanya katika vikundi vya maelfu chini ya majemadari wao na kuweka wakubwa kwa kuwaongoza; na vikundi vya mamia, navyo vikiongozwa na wakubwa wao.
Daudi alikuwa ameikaa kati ya milango miwili ya muji. Naye mulinzi wa mulango akapanda juu ya ukuta mpaka juu ya mulango na alipoinua macho yake aliona mutu akikimbia peke yake.
Mufalme akawaamuru Yoabu, Abisayi na Itayi: “Kwa ajili yangu, mumutendee yule kijana Abusaloma kwa upole.” Watu wote walimusikia mufalme alipoamuru wakubwa wake juu ya Abusaloma.
Wakubwa watano wa Wafilistini walipokuwa wakipita na makundi yao ya waaskari ya mamia na maelfu, Daudi naye akiwa na watu wake pamoja na Akisi walikuwa wanafuata upande wa nyuma wa kundi lile.