Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:28
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.


akisema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Yawe ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja mpaka kwa jamaa ya bwana wangu!”


Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


Huyo mwanamuke kutoka Tekoa akaenda kwa mufalme, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme, akamwambia: “Ee mufalme, unisaidie.”


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Siku ya ine wakakusanyika katika Bonde la Sifa, na kumusifu Yawe kwa yote aliyowafanyia. Hii ndiyo sababu bonde hilo linaitwa Bonde la Sifa mpaka hivi leo.


Si sisi, ee Yawe, si sisi; lakini wewe peke yako utukuzwe, kwa ajili ya wema na uaminifu wako.


Yawe atukuzwe! Hakutuachilia katika meno yao.


Nitashangilia na kufurahia wema wako, maana wewe unaona taabu yangu, unajua huzuni yangu.


Yetro akasema: “Atukuzwe Yawe ambaye amewaokoa toka katika mikono ya Wamisri na kutoka katika mukono wa mufalme wa Misri.


Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.


Kisha akamwambia Daudi: “Wewe una haki kuliko mimi; umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa mabaya.


Abigaili alipomwona tu Daudi, akashuka mara moja kutoka juu ya punda wake, na kuinama mbele ya Daudi mpaka uso wake ukagusa chini.


Abisai akamwambia Daudi: “Leo Mungu amemutia adui yako katika mikono yako. Basi, uniache nimushindilie katika udongo kwa pigo moja tu la mukuki. Sitamupiga mara mbili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ