Halafu Yoabu akamwambia mutu mumoja wa inchi ya Etiopia: “Wewe, uende umwelezee mufalme yale uliyoona.” Mwetiopia yule akainama kwa heshima mbele ya Yoabu, akaondoka mbio.
Daudi alikuwa ameikaa kati ya milango miwili ya muji. Naye mulinzi wa mulango akapanda juu ya ukuta mpaka juu ya mulango na alipoinua macho yake aliona mutu akikimbia peke yake.